Waathirika mabomu Gongo la Mboto kukabidhiwa nyumba leo

Milipuko ya mabomu Gongo la Mboto




Na Mwandishi wetu

Rais  Jakaya Kikwete, leo anatarajiwa kukabidhi nyumba 36 kwa waathirika wa mabomu ya Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Meck Sadiki, Rais Kikwete atakabidhi nyumba hizo zilizojengwa na Serikali katika maeneo ya Msongola Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Sadiki alisema makabidhiano hayo yatafanyika katika maeneo hayo kuanzia mchana.

Februari 18, mwaka jana, ilitokea milipuko ya mabomu katika kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) iliyoko Gongo la Mboto na kusababisha vifo vya watu takribani 30 na wengine 600 kujeruhiwa.

Watu kadhaa walikosa makazi baada ya nyumba zao kuharibiwa.

Taarifa ya tathmini ya athari za nyumba ilionyesha kuwa nyumba 77 ziliharibika kabisa na 1,748 ziliharibika kidogo.

Post a Comment

0 Comments