Ngassa kiini cha burudani Taifa leo

Mrisho Ngassa
Sosthenes Nyoni
WINGA
Mrisho Ngassa wa Simba, leo anatarajia kuwa kiini cha utamu wa mchezo
wa soka, pale atakaipoikabili kwa mara ya kwanza timu yake ya zamani,
Azam FC katika mechi ya Ngao ya Jamii, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Simba,
mabingwa wa soka Bara walimsajili Ngassa kutoka kwa washindi hao wa
pili wa Ligi Kuu Azam. Kabla ya kutua Simba, Ngassa alikuwa akiwaniwa na
Yanga ya Dar es Salaam.
Mbali na Ngassa, mwingine ambaye leo huenda akawa kivutio, ni Ramadhan Chombo 'Redondo' atakayekuwa na timu yake mpya Simba.
Redondo
ambaye usajili wake ulizua utata, alisajiliwa na Simba kutoka Azam FC,
ambao nao awali walimsajili kutoka kwa Wekundu hao wa Msimbazi.
Pambano
la timu hizo ni ishara ya kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu mwishoni
mwa wiki hii, kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
REKODI
Kwa
mwaka huu pekee, Simba na Azam zimekutana mara tano katika mechi za
mashindano mbalimbali. Hazijawahi kutoka sare, huku Simba ikishinda
michezo mitatu na Azam miwili.
Mechi ya karibuni ni ile ya nusu
fainali ya michuano ya Super8, ambapo Simba iliyochezesha kikosi 'B'
dhidi ya kikosi kamili cha Azam, ilishinda mabao 2-1.
Vikosi:
Kwa kiasi kikubwa Simba itakuwa na mwonekano tofauti kwa vile ina sura kadhaa mpya kutoka ndani na nje ya nchi.
Miongoni
mwa nyota wapya mbali na Redondo na Ngassa kwenye jeshi la Simba leo,
wengine ni mshambuliaji wake mpya kutoka Ghana, Daniel Akufo na beki
raia wa Mali Komanbill Keita na Mkenya, Pascal Ochieng.
Nayo Azam
kama ilivyo kwa wenzao wa Simba, inatarajiwa kuwa na mabadiliko kidogo
hasa hasa katika mpangilio wa kikosi na hii ikitokana na kutokuwapo kwa
Ngassa na Redondo.
Mfumo:
Wakati Simba itakuwa na kocha
mwenye uzoefu na timu hiyo Milovan Cirkovic, Azam itaongozwa na kocha
wake mpya Boris Bunjak aliyeukwaa ubosi, baada ya kutimuliwa Mwingereza
Stewart Hall.
Timu zote zinatumia mfumo mmoja wa 4-4-2 na hata aina ya soka lao pia linafanana, likipingwa pasi nyingi fupifupi.
Wakizungumzia
pambano baina yao, makocha wa timu hizo wakiwa katika hali ya kujiamini
walijinasibu kila moja kufanya kweli na kuibuka na ushindi.
"Itakuwa
mechi ngumu, lakini ni wakati wa sisi kulipa kisasi baada ya wao
kutufunga Kombe la Kagame. Tupo vizuri kiakili na kisaikolojia," alisema
Cirkovic.
Naye Bunjak alisema, "Ili ushinde unahitaji
maandalizi, na kwa upande wetu tumejiandaa kikamilifu kuhakikisha
tunashinda mechi hiyo na kutuongezea morali katika ligi."
Kwa
upande mwingine, wachezaji wa kuchungwa zaidi leo ni pamoja na
mshambuliaji nyota wa Simba Mganda Emmanue Okwi, kama itakavyokuwa kwa
mpachika mabao hatari wa Azam John Boko 'Adebayor'.
Rekodi kamili Simba/ Azam mwaka 2012.
Mapinduzi Cup: Azam 2-0 Simba
Ligi Kuu: Simba 2-0 Azam
Urafiki Cup: Simba 3 -1 Azam (pen)
Kagame Cup: Azam 3- 1 Simba
Super 8: Simba 2- 1 Azam.
Wachovu Liverpool wauvaa muziki wa Man City
LONDON, England
MABINGWA wa England, Manchester City kesho watashuka kwenye Uwanja wa Anfield kuwavaa wachovu Liverpool.
Manchester
City wataingia uwanjani huku wakiwa na rekodi nzuri ya ushindi wa mabao
3-2 waliopata dhidi Southampton wiki iliyopita ukiwa ni ushindi wa tano
katika mechi tano za karibuni.
Wapinzani wao, Liverpool wakiwa
mbele ya mashabiki wao watakuwa na jukumu moja la kuhakikisha
wanarudisha imani kwa mashabiki wao baada ya kuchapwa 3-0 na West Brom
kwenye mchezo uliopita.
 |
Man City
|
Manchester City inakwenda katika mechi
hiyo ikiwa na historia nzuri katika siku za karibuni, lakini timu hizo
zilipokutana katika mechi tano za nyuma, Liverpool ilipata ushindi mara
mbili, Manchester City mara moja na walitoka sare katika mechi mbili.
Liverpool
haitakuwa na beki Daniel Agger, ambaye amefungiwa mechi moja na
Machester City itawakosa wachezaji watatu majeruhi ambao ni mshambuliaji
Sergio Aguero, kiungo Gareth Barry na beki Micah Richards.
Ukiachilia
mbali mechi hiyo, Manchester United ambayo Jumatatu wiki hii
ilikaribishwa katika ligi kwa kichapo cha bao 1-0 kutoka Everton huenda
ikazinduka wakati itakapokutana na Fulham leo.
Manchester United iliyosajili Shinji Kagawa na Robin van Persie, ilishindwa kutamba mbele ya Everton.
Baada
ya mechi hyo kocha, Alex Ferguson alikiri alifanya makosa kutomwanzisha
Van Persie na badala yake nyota huyo aliingia uwanjani dakika 22 kabla
ya kipenga cha mwisho.
Hata hivyo, wapinzani wao Fulham wapo
katika hali nzuri baada ya kuisambatisha Norwich City mabao 5-0 katika
mechi ya fungua dimba.
Nayo Chelsea itakuwa na wakati mgumu
itakapoivaa Newcastle leo. Katika mechi ya awali, Chelsea iliifunga
Wigan mabao 2-0 na katikati ya wiki hii waliinyuka Reading mabao 4-2.
Newcastle
iliyomaliza msimu uliopita katika nafasi ya tano juu ya Chelsea ilianza
ligi kwa kutoa kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Tottenham.
Nayo
Arsenal iliyoanza ligi kwa suluhu dhidi ya Sunderland, itataka kuzinduka
wakati itakapokuwa ugenini kupambana na Stoke City kesho Jumapili
wakati Tottenham itakwaaana na West Brom leo.
Rais Kagame aipa tano Yanga
 |
Wachezaji wa Yanga wakishangilia ushindi wa kutwa kombe la Kagame
|
Doris Maliyaga, Kigali Rwanda
RAIS Paul Kagame wa Rwanda, ameipongeza
klabu ya Yanga kwa kutwaa mara ya pili mfululizo Kombe la Kagame na
kusema mafanikio hayo yanatokana na umoja na mshikamano ndani ya klabu
hiyo.
Kagame, ambaye ni mdhamini mkuu wa mashindano hayo,
alikutana wachezaji wa Yanga na viongozi wao katika hafla aliyowaandalia
kwa ajili ya kuwapongeza iliyofanyika Ikulu ya Kigali Jumatano usiku
wiki hii.
Yanga ilitwaa ubingwa mara ya pili mfululizo baada ya
kuifunga Azam FC 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa, ambapo mwaka jana ilifanya
hivyo pia kwa kuifunga Simba 1-0 kwenye uwanja huohuo.
"Nawapongeza
kwa ushindi wenu. Ni jambo zuri na inaonyesha ni jinsi gani mlivyo na
umoja wa kweli katika michezo," alisema Kagame ambaye katika hafla hiyo
uongozi wa Yanga ulimkabidhi jezi ya timu yao.
"Nataka kuwaambia
neno moja, mafanikio mliyopata ni furaha kwa wote kwa maana sisi sote ni
ndugu. Yanga ni klabu ya Tanzania na Afrika Mashariki, sisi sote ni
wamoja.
"Nawaambieni, leo tunaweza kujiona sisi ni tofauti kwa
sababu ya utaifa wetu, lakini akifuatilia chimbuko la wazee wetu wa
zamani, utagundua sisi ni wamoja kutokana na mchanganyiko wetu,"
alifafanua.
"Kuna Watanzania wengi hapa Rwanda, lakini pia kuna Wanyarwanda wengi Tanzania. Hii inaonyesha ni jinsi gani tulivyo wamoja."
Wakati
huohuo, Kocha wa Yanga, Thomas Saintfiet ameahidi kukirudisha kikosi
chake mjini Kigali kupiga kambi baada ya kufurahishwa na mazingira ya
mji huo.
Yanga imeweka kambi katika Hoteli ya La Pallise iliyopo
eneo la Remera kujiandaa na michuano ya Ligi Kuu Bara inayotarajiwa
kuanza baadaye mwezi ujao.
"Hii ni mara yangu ya kwanza kufika
Rwanda, lakini hakika nimefurahishwa na mazingira ya hapa, naahidi
nitarudi tena kuweka kambi na timu yangu," alisema Saintfiet mbele ya
Rais Kagame.
"Nitafanya hivyo lakini pia huenda nikaleta tena
kombe hili kwa mara nyingine kwa maana mazingira ni tulivu na mazuri,
kila kitu kinaenda sawa,"alisema Saintifiet.
0 Comments