Mariam 'Mapepe' wa TOT afariki dunia

Aliyekuwa Mwimbaji nyota wa kundi la TOT

 - Taarab, Mariam Hamis 'Mapepe'


 Na Sabato Kasika

Mwimbaji nyota wa kundi la TOT - Taarab, Mariam Hamis 'Mapepe', aliyetamba na wimbo wa "Paka Mapepe", amefariki dunia usiku wa kuamkia jana wakati akijifungua ambapo anatarajiwa kuzikwa leo katika makaburi ya Magomeni jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa katibu wa kundi la TOT, Gasper Tumaini, mwimbaji huyo alikutwa na mauti katika hospitali ya Mwananyamala ambapo mtoto yuko hai.

Tumaini alisema kuwa msiba upo nyumbani kwao marehemu eneo la Magomeni Makuti wakati mipango ya mazishi ikiendelea na anatarajiwa kuzikwa leo jioni.

"Tumepoteza mmoja wa waimbaji nyota wa TOT-Taarab ambaye alikuwa akitegemewa na kundi letu kwa umahiri wake katika uimbaji," alisema Tumaini.

Akifafanua zaidi, alisema Mariam alijiunga na TOT-Taarab mwaka jana akitokea Five Star Modern Taarab ambapo alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa kundi hilo ambalo baadaye lilipata ajali na kupoteza baadhi ya wasanii wake.

Alisema kuwa mchango wake ulikuwa mkubwa kutokana na uwezo wa kuimba aliojaliwa na mwenyezi Mungu pamoja na ushirikiano aliouonyesha kwa wasanii wenzake.

Enzi ya uhai wake alianza kusikika kwenye muziki wa mwambao akiwa na kundi la Zanzibar Stars na baadaye akahamia East African Melody kabla ya kwenda Five Star na kisha TOT- Taarab ambako hadi anafariki alikuwa akifa
nya kazi.

Post a Comment

0 Comments