Loliondo ‘ya Kigamboni’; Ardhi mbichi, ukahaba -2

Mandhari ya eneo la Loliondo kama ilivyokutwa wakati wa ziara ya Mwananchi


“Wanawake hao huvutia biashara kwa kuwatoza wateja wao Sh1,000  kwa anayependa kushika maziwa na Sh1,500 hadi  10,000   kwingineko na kitendo kikamilifu huwa ni makubaliano na huanzia Sh 10,000 na kuendelea.”

 

JUHUDI  na harakati za kuzungumza na mwanamke  kiongozi  wa kundi hilo  hazikuwa rahisi. Ilikuwa lazima kwetu kujitambulisha kuwa tunatoka taasisi binafsi ya kusaidia wanawake.

 

Kiongozi huyo, Mama Nasra anasema  yeye na mabinti zake hao, wapo hapo kwa ajili ya biashara nyingi, kwanza ni gongo, bangi, sigara na ‘mengineyo’.

 

Anasema  baadhi ya binti  zake hawafanyi  biashara hiyo kwa njaa, kwani wapo waliotoroka majumbani kwao ambako walikuwa wakisoma na kupewa mahitaji yote muhimu.

 

“Kwa wengine hiki  ni kipaji tu au hulka. Hao watoto wengine walikuwa wanasoma. Wanapenda wenyewe kufanya kazi hiyo,” anasema.

 

Anaongeza kuwa hata yeye si maskini na anamiliki nyumba ya vyumba vitano na sebule maeneo ya Mbagala Rangi Tatu, mali ambayo ameipata kwa biashara hizo hizo.



Kuhusu kuuza gongo, anasema anaona pombe hiyo, pamoja na bangi vina faida zaidi kuliko bia.

 

Anasema alishawahi kujaribu biashara ya kuuza bia, lakini hakuona faida ukilinganisha na faida anayopata kwa kuuza pombe za kienyeji.

 

Akiwa ameshika pakiti ya sigara, mwanamke huyo anaeleza kuwa anawalea wasichana hao na wanashiriki pamoja katika kufanya biashara.

 

“Halafu sisi si wakaaji hapa, siku mbili tatu tunahamia kambi nyingine, umeshanisoma,” anasema huku akiendelea kuchomoa sigara na kuwapa wateja wake.

 

Wakati tukiendelea kuzungumza, binti mmoja mweupe ambaye anaonekana amelewa anaelekea katika shamba la mahindi na mwanaume aliyeketi naye awali.

 

Hata hivyo, mwanamke huyo anawazuia wasichana wake kuzungumza lolote na kuwaamuru waondoke katika eneo hilo mara moja.

 

Anasema: “Si unawaona hao, ‘wamepinda’, hao usiwaone hivyo, wameshashindikana makwao,”

 

Kwa upande wao, vijana walionipeleka eneo hilo wananihakikishia  kuwa huo ni mchana tu …usiku mambo huwa moto zaidi.

Post a Comment

0 Comments