Mauaji na Ubakaji Sudan Kusini

Wanajeshi wa Sudan Kusini


Ripoti ya Shirika la Amnesty International imefichua kuwa Wanajeshi wa Sudan Kusini wanaoendeleza zoezi la kuwapokonya wenyeji silaha haramu mashariki mwa nchi hiyo, wanatumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia.

Shirika hilo linasema Wanajeshi hao wanafanya vitendo vya mauaji na ubakaji.

Serikali ilizindua zoezi hilo katika juhudi za kurudisha amani mapema mwaka huu kufuatia mapigano ya kikabila yaliyozuka katika Jimbo la Jonglei ambako mamia ya watu waliuawa.

 

Hata hivyo, visa vya mateso na unyanyasaji vimeripotiwa kutoka kwa Wanajeshi na Polisi wanaosaka Silaha haramu zinazotumika kwenye mapigano hayo.

 

Mwandishi wa BBC amesema kwamba hapo awali Serikali ilipuuza tetesi kuhusiana na visa hivyo vya mateso na unyanyasaji tangu Taifa changa la Sudan Kusini lilipojinyakulia uhuru wake zaidi ya mwaka mmoja uliopita

Post a Comment

0 Comments