Mahakama yamweka Lulu 'Kitanzini'


Msanii wa fani ya Filamu nchini Elizabeth Michael 'Lulu'
 

  *Sasa kutinga Kisutu Jumatatu

Jopo la Majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa imeamua kusitisha uamuzi wa Mahakama Kuu ya kutaka kuchunguza umri wa Msanii wa fani ya Filamu nchini Elizabeth Michael maarufu kama Lulu na badala yake imeelekeza jalada la kesi lirudi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuendea na kesi ya msingi.

Maamuzi hayo yalifikiwa baada ya jopo la majaji hao wa Mahakama hiyo kusikiliza hoja za pande zote mbili kufuatia  maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na upande wa mashitaka ukiomba mahakama hiyo ifanye marejeo ya uamuzi wa Mahakama Kuu.

Juni mwaka huu, Mahakama Kuu ilikubali kufanya uchunguzi wa umri halali wa mshitakiwa huyo,  kufuatia maombi yaliyowasilishwa mahakamani hapo na jopo la mawakili wanaomtetea Mshitakiwa huyo.

Akisoma maamuzi yaliyofikiwa na jopo hilo jana jijini Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Zahra Maruma,alisema kuwa Jaji Dk. Fauz Twaibu hakuwa na mamlaka ya kutenda alivyotenda kwani alitumia nguvu zake za marejeo katika kutaka mahakama yake ichunguze umri wa mshitakiwa.

Alisema hata katika marejeo yao hayakuwa sahihi kwani bado kulikuwa na makosa katika hilo na kwamba upande wa Jamhuri haukutoa sababu za kuomba marejeo katika mahakama ya Rufaa.

Maruma alisema Jaji Dk. Fauz  alikosea kufanya maamuzi kwa mujibu wa kifunga cha sheria alichokitumia cha kutaka umri wa  mshitakiwa kuchunguzwa na Mahakama Kuu.

Alisema kama palikuwa na mapungufu alitakiwa kurudisha jadala hilo  likiwa na maelekezo katika Mahakama ya Haklimu Mkazi Kisutu na sio kutoa maamuzi ya kutaka umri wa mshitakiwa kuchunguzwa.

Maruma alisema kesi hiyo itaendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisitu mpaka hapo upelelezi utakapokamili.

Kwa upande wake wakili anayemtetea mshitakiwa huyo, Peter Kibakara,alisema wamekubaliana na maamuzi hayo ya kurudi katika mahakama ya kisuti kwa ajili ya kuendelea kwa shauri hilo.

Lulu anakabiliwa na kesi ya mauaji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akituhumiwa kumuua msanii mwenzake, Steven Kanumba. Anadaiwa kutenda kosa hilo April 7 mwaka huu  nyumbani kwa marehemu, Sinza jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, umri wake umezua mvutano mkali baina ya upande wa mashitaka katika kesi hiyo na jopo la mawakili wanaomtetea mshitakiwa huyo, hali ambayo mvutano huo ulipelekea kufikia ngazi ya Mahakama ya Rufaa ikiwa kesi ya msingi bado haijaanza kusikilizwa.

Awali utata huo ulitokea pale ilipodaiwa umri wa mshitakiwa ni chini ya miaka 18 na kwamba kesi hiyo ilitakiwa kusikilizwa katika Mahakama ya watoto na sio katika Mahakama ya Kisutu huku upande wa mashitaka ukidai umri wa mshitakiwa ni zaidi ya miaka 18.

Vielelezo vilivyowasilishwa Mahakamani Kuu na upande wa mashitaka ambavyo ni hati za viapo vya wazazi wa mshitakiwa ambao ni Lucresia Kalugila na Michael Kimemeta ikiwemo cheti cha kuzaliwa na cha ubatizo vikionyesha umri wake ni miaka 17.

Hata hivyo, vielelzo vilieleza kuwa mshitakiwa huyo alizaliwa April 16 mwaka 1995 katika kituo cha afya Muhimbili na kupewa cheti cha kuzaliwa namba B.0318479 cha Julai 23 mwaka 2004.

Lakini vielelezo vya upande wa mashtaka vilionyesha mshitakiwa huyo ana umri zaidi ya miaka 18  vielelezi hivyo ni pamoja na maelezo ya mshitakiwa alivyoitwa polisi wakati alipohojiwa kuhusiana na tuhuma zinazomkabili, maombi ya hati ya kusafiria na maombi la leseni ya udereva.

Pia kuna mkanda wa video aina ya CD ya mahujiano kati ya mshitakiwa na mtangazaji wa kituo kimoja cha runinga nchini.
Hivyo kesi hiyo inatarajiwa kutajwa Oktoba 8 mwaka huu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
Kumbukumbu muhimu za shauri la Lulu:

Aprili 7, 2012: Steven Kanumba anafariki dunia, Lulu anadaiwa kusababisha kifo hicho.

Aprili 11, 2012: Lulu anafikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, ikiwa ni mara ya kwanza tangu kifo cha Kanumba kutokea.

Mei 28, 2012: Utata wa umri wa Lulu waanza kuibuliwa mahakamani.

Julai 9, 2012: Shauri la utata kuhusu umri wa Lulu kuwasilishwa mahakamani.

Oktoba 5, 2012: Mahakama ya Rufaa yabainisha Lulu anastahili kushitakiwa

Post a Comment

0 Comments