Ajali ya basi la Super Feo yaua


Na Nathan Mtega

Raia wawili wa Kenya wamefariki dunia papo hapo na wengine watatu wamejeruhiwa vibaya baada ya magari mawili waliyokuwa wakisafiria aina ya Canter kuligoga basi la abiria mali ya kampuni ya Super Feo lililokuwa likitoka Songea kuelekea Dar es Salaam.
 
Habari zilizopatikana mjini Songea mkoani Ruvuma zimedai kuwa ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 3:00 asubuhi katika kijiji cha Wino wilayani Songea karibu na mpaka wa Mkoa wa Ruvuma na Njombe na watu wawili waliokuwa kwenye Canter ambao ni dereva na utingo wake walifariki dunia papo hapo baada ya gari hilo kugongana na basi hilo.
 
Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo, majeruhi watatu ambao walikuwa ni abiria wa basi la Super Feo ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja walikimbizwa katika Hospitali ya Serikali ya Wilaya ya Njombe kwa matibabu zaidi huku miili ya marehemu wawili wa ajali hiyo ikihifadhiwa katika kituo cha afya cha Madaba wilayani Songea.
 
Walieleza kuwa Canetr iliyokuwa imesheni nyama ya kuku pamoja na mayai ilikitokea wilayani Mufindi, mkoani Iringa ikiwa kwenye mwendo kasii kwenye na iligongana na basi hilo ambalo lilikuwa likitoka Songea kuelekea Dar es Salaam na baadaye basi hilo liliendelea na safari.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Deusdedit Nsimeki, alithibitisha kutokea kwa  ajali hiyo na kusababisha vifo raia hao wa Kenya na majeruhi watatu.

Post a Comment

0 Comments