Mwandosya, Slaa ‘wagawana’ watoto wa hayati Mwangosi

Mjane wa Daudi Mwangosi aliyekuwa mwandishi wa Channel Ten,Itika akilia kwa uchungu juu ya kaburi la mumewe kwenye mazishi yaliyofanyika kijijini kwake Kasoka wilayani Rungwe mkoani Mbeya jana.Picha kwa hisani ya mbeyayetu.blogspot.com


KILA MMOJA AJITWISHA JUKUMU LA KUWASOMESHA, WAPIGANA VIJEMBE KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2015

Hawa Mathias, Mbeya na Tumaini Msowoya, Iringa

MAZISHI ya Mwandishi wa Habari, Daud Mwangosi yalifanyika jana katika Kijiji cha Busoka kilichoko wilayani Rungwe, Mbeya na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa. Katika mazishi hayo, viongozi hao wawili kila mmoja alitangaza kuwasomesha watoto wa marehemu Mwangosi ambaye alifariki dunia Septemba 2, mwaka huu baada ya kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu wakati polisi walipokuwa wakisambaratisha mkutano wa Chadema.


Akitoa salamu zake katika mazishi hayo, Profesa Mwandosya alisema yupo tayari kumsomesha mtoto wa kwanza kati ya wanne wa Mwangosi, Nehemia ambaye anasoma kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Malangali.

Alisema atamsomesha mtoto huyo kidato cha tano na sita na ikiwa atafaulu na kukosa mkopo wa elimu ya juu, atamsomesha mpaka atakapomaliza elimu yake ya juu.


Dk Slaa kwa upande wake, alisema amewasiliana na rafiki yake ambaye yupo tayari kuwasomesha watoto wawili wa Mwangosi ambao wote wapo shule ya msingi. Mtoto wa mwisho wa marehemu hajaanza masomo.

Pamoja na kuwasomesha watoto hao, alisema Chadema kimetoa Sh2 milioni za rambirambi kutokana na msiba huo.


Vijembe msibani

Awali, Profesa Mwandosya na Dk Slaa walitoa kauli zinazoonyesha kupigana vijembe vya kisiasa, baada ya waziri huyo kumtaka Dk Slaa aache kufanya kampeni za kuingia Ikulu mwaka 2015 msibani.

Kauli hiyo ya Profesa Mwandosya ilikuja baada ya Dk Slaa kutaka polisi waliohusika na mauaji hayo wachukuliwe hatua za kisheria kwa sababu wanajulikana.


“Tunashangaa wamekamatwa watu wengine na kuwaacha waliohusika na mauaji hayo, tunawajua kwa sababu wameonekana hadharani, hakuna siri kwa hilo,” alisema Dk Slaa.


Akizungumza baada ya kauli hiyo ya Dk Slaa, Profesa Mwandosya aliwataka wanasiasa wa vyama vya upinzani kuacha kutumia misiba kutafuta kura za urais mwaka 2015.


“Natoa pole sana kwa familia na tasnia nzima ya habari nchini. Hiki ni kipindi kigumu, lakini tuviachie vyombo husika vifanye uchunguzi wa mauaji haya,” alisema Profesa Mwandosya na kuongeza:

“Lakini nichukue fursa hii kuwaomba wanasiasa waache kutumia misiba ili kujipatia umaarufu katika kutafuta kura za urais mwaka 2015.”


Katika mahubiri yake msibani hapo, Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Busoka, Mathayo Mwanjemele alikemea mauaji hayo na kuwaomba wahusika wajitokeze hadharani kabla Mungu hajawaumbua.

“Waliohusika na mauaji haya wajitokeze na kutubu kwa wananchi kabla adhabu ya Mungu haijawakuta,” alisema.

Alisema ufike wakati Serikali iwe inakiri uzembe unaofanywa na watendaji wake ambao umekuwa ukitokea mara kadhaa.


IGP Mwema asimamia uchunguzi
Kabla ya mazishi hayo, mwili wa Mwangosi ulifanyiwa uchunguzi na wataalamu wa afya kutoka Dar es Salaam, huku IGP Said Mwema akishuhudia.


Baada ya kumalizika uchunguzi huo, usiku mwili wa marehemu ulisafirishwa kuelekea Mbeya kwa mazishi.

Mwili huo ulipofika Tukuyu, umati mkubwa ulijipanga barabarani na kupunga mkono, huku wengine wakiusindikiza kwa baiskeli na pikipiki hadi kijijini, Busoka.


Majeruhi wengine 

 Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mafinga, Dk Peter Mwenda alisema mbali na marehemu Mwangosi, watu wengine 10 walijeruhiwa, wawili kati yao walitibiwa na kuruhusiwa. Alisema waliobaki hospitalini hapo hali zao zinaendelea vizuri.


Aliwataja majeruhi hao kuwa ni Hussein Kweha (27), Edson Iddy (22), Alfred Kibitanyi (27), Hamad Musa (37), Yeremia Kulwa (45) na Christopher Pesa (30).


Alisema majeruhi hao walidai kwamba walikuwa katika mkutano wa ndani wa Chadema na askari waliwataka kutulia kabla ya kuwashambulia kwa marungu na vitu vyenye ncha kali.

Pata habari na picha zaidi: kwa hisani ya Mbeyayetu.blogspot.com

UPDATES!! TUKIO ZIMA LA MAZISHI(SAFARI YA MWISHO) LA MPIGANAJI MWANDISHI WA CHANEL TEN DAUDI MWANGOSI, TUKUYU MBEYA.

 Waandishi wa Habari wakiwa wamebeba Mwili wa Marehemu kuelekea Makaburini
Wakiwa wanafanya ibada ya Mwisho kabla ya kuanza maziko
Hapa wakiwa wanashusha mwili wa marehemu katika Nyumba yake ya milele
Mwili wa Marehemu Daudi Mwangosi ukiwa Tayari katika Kaburi
Shughuli za kuzika zimeanza
 Mazishi yanaendelea 
 Mke wa Marehemu Daudi Mwangosi akiweka Shada la Mauwa kwa machungu
 Mke wa Daudi Mwangosi akiwa analia kwa uchungu katika Kaburi la Marehemu Mumewe 


 Watoto wa Marehemu wakiwawanaweka mashada ya maua sasa 
Ni ngumu sana Kuamini kwa mke wa Marehemu lakini hali ndivyo ilivyo kuwa akiwa na huzuni kubwa
 Dr Slaa akiweka Shada la Mauwa 
Dr Slaa Baada ya kumaliza kutoa heshima za mwisho
Mh. Mark Mwandosya akiweka Taji la maua pamoja na mke wake 
 Rais wa UTPC akiweka shada la Maua
 Ndugu wa Marehemu akiweka shada la Maua

Mwenyekiti wa Mbeya Press Club akiweka shada la maua 
Mwandishi Mkuu wa Mbeya  yetu, Ndugu Joseph Mwaisango akiwa anatoa heshima zake za Mwisho katika Kaburi
Wananchi wakiwa wanarejea baada ya mazishi

Waandishi wa Habari wakichukua Tukio Live `
Na huu Ndio Mwisho wa tukio zima la Mazishi ya Ndugu yetu, Mwanaharakati, Mpiganaji Daudi Mwangosi aliyekuwa Mwandishi wa Chanel 10.


Mpiga picha Mkuu alikuwa ni Ndugu Joseph Mwaisango

Updates! Hivi ndivyo zilivyo kuwa shughuli nzima za kuuaga Mwili wa Marehemu Daudi Mwangosi Itete Tukuyu Mkoani Mbeya

 Mwili wa Marehemu Daudi Mwangosi ukiwa una andaliwa kwa ajili ya kutolewa Heshima za mwisho
 Mheshimiwa Mark Mwandosya akitoa Heshima za Mwisho
 Muheshimiwa Dr Slaa akitoa Heshima za mwisho

 Ndugu jamaa na Marafiki wakitoa Heshima za Mwisho
Mke wa Marehemu akitoa heshima zake za Mwisho
 Ma elfu ya watu wakipita kutoa Heshima zao za mwisho
 Huko Jikoni Mambo yanaendelea 
 Mama Mzazi wa Marehemu Daudi Mwangosi akiwa analia kwa Uchungu

Dr Slaa akiwa pamoja na Mh. Mark Mwandosya

Live! Salam pamoja na Ibada ya Mazishi imeanza sasa Itete Tukuyu mkoani Mbeya katika mazishi ya Mwandishi wa Habari Daudi Mwangosi

Mke wa Marehemu Daudi Mwangosi akilia kwa Uchungu Muda huu
 Maelfu ya  watu wakiongezeka kuja katika Mazishi ya mwandishi wa habari wa Chanel 10 Daudi Mwangosi Muda huu
 Mheshimiwa Mark Mwandosya ambaye ni Waziri ofisi ya Rais na pia Mbunge wa Rungwe Mashariki akitoa salam kwa Niaba ya Serikali
 Watu wakiwa wengi na wenye utulivu wakisikiliaza watu mbalimbali wakitoa salam zao kwa ndugu wa Marehemu
 Mjane Mke wa Marehemu Daudi Mwangosi aliye jishika, akiwa na uchungu muda huu
Ibada ikiwa inakaribia kuanza
 Ibada ya mazishi ndio imeanza muda huu
 Baadhi ya Waandishi wa Habari wakiwa wenye majonzi Makubwa
Waandishi wa Habari wakiwa katika msiba wa kwanza kutoka kulia ni Ndugu Joseph Mwaisango ambaye ni mwandishi mkuu wa Mbeya yetu Blog, Rais wa UTPC Keny Simabaya, pamoja na Felix Mwakyembe .


Liveee!! Tukio Mazishi ya Mwandishi wa Habari wa Chanel 10 Daudi Mwangosi kijijini Kwao Itete Tukuyu Mkoani Mbeya

 Wawakilishi Mbalimbali wakitoa salam za Pole kwa ndugu wa Marehemu
 Mwakilishi wa Chanel Ten Hamis akitoa pole katika msiba huu muda huu

 Mwenyekiti wa Mbeya Press Club akitoa pole zake kwa wafiwa 
 Mwanaharakati Francis Godwin akielezea Jinsi Mauti yalivyo mkuta Mwandishi wa Habari Daudi Mwangosi

Rais wa UTPC Kenny Simbaya ambaye pia ni kiongozi wa msafala wa kuleta Mwili wa Marehemu Daudi Mwangosi akiwa anatoa salam za Pole kwa wafiwa.
Dr  Slaa akitoa pole kwa wafiwa wote Muda huu



Wakina mama wakiwa wenye majonzi makubwa sana na huzuni muda huu

picha zote kwa hisani ya mbeyayetu.blogspot.com
 Tunawashukuru sana uongozi mzima wa mbeyayetu.blogspot.com
kwa kutupatia matukio haya live. HVP Studio tunawapongeza kwa kazi nzuri na ngumu uliyoifanya

Post a Comment

0 Comments