Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wawaomba radhi Watanzania

kwa mujibu wa Mh. Mo Dewji blog, wasanii wa Bongo Movie ambao ni maadhi ya mastaa maafuru nchini, Wema Sepetu na Aunt Ezekiel, wamekutana na waandishi wa habari kwa lengo la kuomba radhi Watanzania kufuatia picha za “utata” walizopigwa wakati wa Tamasha la Serengeti Fiesta lililofanyika Dodoma. Picha hizo zilisababisha baadhi ya watu na blogs kulalamika kwamba walikua wako “nusu uchi.”

“Kiukweli hatujafurahia na tumeumia sana na tunatumia fursa hii kuomba Msamaha.” Wema Sepetu alikaririwa akisema na Mh. Mo Dewji blog. Zifuatazo ni baadhi ya picha za tukio hilo. Aunty Ezekiel alisisitiza kwamba wameumia sana kwa kuonekana kwa picha zile kwa sababu wao kama wanawake katika jamii, wana wazazi, Ndugu, jamaa, marafiki pamoja na mashabiki mbalimbali wa kazi zao ambao wanawaheshimu kuliko baadhi ya watu wanavyofikiria. Picha na habari kutoka :Mo Dewji Blog. Zifuatazo ni picha kutoka kwenye mkutano huo:

wema sepetu aunt ezekiel waomba radhi watanzania 00 Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wawaomba radhi Watanzania

“Kiukweli hatujafurahia na tumeumia sana, na tunatumia fursa hii kuomba Msamaha.” – Wema Sepetu

wema sepetu aunt ezekiel waomba radhi watanzania Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wawaomba radhi Watanzania

Wema Sepetu akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Msanii wa Bongo Movie Aunt Ezekiel na kushoto Katibu Mkuu wa TAFF Wilson Makubi.

wema sepetu aunt ezekiel waomba radhi watanzania 0 Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wawaomba radhi Watanzania

Aunt Ezekiel akizungumza na waandishi wa habari

wema sepetu aunt ezekiel waomba radhi watanzania 1 Wema Sepetu na Aunt Ezekiel wawaomba radhi Watanzania

Baadhi ya picha hizo zilizopelekea wasanii hao kuomba radhi. Pichani wasanii Aunty Ezekiel na Steven Nyerere (Kulia )

Post a Comment

0 Comments